Nyota wa zamani wa Arsenal Emmanuel Petit ameionya klabu yake ya zamani dhidi ya kumsajili mshambuliaji wa Newcastle Alexander Isak msimu huu wa joto.

The Gunners walikuwa na nia ya kumsajili mchezaji huyo wa kimataifa wa Uswisi miaka miwili iliyopita alipokuwa akiichezea Real Sociedad ya Uhispania.

Arsenal hawakuwa tayari kufikia bei inayotakiwa na klabu hiyo ya La Liga na mshambuliaji huyo mwenye kipaji kikubwa hatimaye alihamia Newcastle msimu uliofuata.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 tangu wakati huo amejijengea sifa ya kuwa mmoja wa wafungaji bora wa Ligi kuu Uingereza na amefunga mabao 19 katika mashindano yote.

Arsenal walivunja rekodi yao ya usajili msimu uliopita wa joto ili kumnunua Declan Rice, lakini Petit anahofia kuwa Arsenal watafanya makosa makubwa iwapo watatumia kiasi kama hicho walichotumia kumnunua Rice ili kumnunua Isak.

‘Pauni milioni 100 kwa Alexander Isak? Haya… Kutumia kiasi hicho cha pesa kwa mtu kama Declan Rice inaeleweka kwa sababu ina uhakika kwamba Rice atafanya vyema na kuweka juhudi. Sina hakika sana na Isak.

‘Sidhani kama itakuwa uamuzi mzuri kwa Arsenal kumnunua Isak kwa bei kubwa. Sera ya uhamisho ya Arsenal ni nzuri sana' Alisema Petit







You Might Also Like

Get Newsletter

Advertisement