Newcastle United wanahofia huenda wakahitaji kumuuza kiungo wa Brazil Bruno Guimaraes, 26, ili kukidhi sheria za kifedha za Ligi ya England. Miamba wa Ufaransa Paris St-Germain wanaongoza katika mbio hizo, huku Manchester United na Arsenal pia wakiwa na hamu.

Tottenham pia wameungana na Arsenal katika kinyang'anyiro cha kumsajili mshambuliaji wa Uswidi Alexander Isak, 24, iwapo Newcastle italazimika kuuza wachezaji wake muhimu msimu huu wa joto.

Lakini Isak amesisitiza kujitolea kwake kwa Newcastle huku kukiwa na nia ya kumsajili wapinzani wa klabu yake ya Ligi ya Premia. 

Newcastle itapatia kipaumbele usajili wa mabeki wawili wakati dirisha la uhamisho litakapofunguliwa baada ya Mholanzi Sven Botman, 24, na Muingereza Jamaal Lascelles, 30, kukabiliwa na majeraha ya muda mrefu.


You Might Also Like

Get Newsletter

Advertisement