Manchester City wana silaha ya siri ya kumsajili Claudio Echeverri, City wanaripotiwa kumenyana na Real Madrid na Barcelona kumnasa kinda wa Argentina Claudio Echeverri, aliyeng'ara kwenye Kombe la Dunia la Vijana chini ya miaka 17.

Lakini uhusiano wa City na River Plate- na vilabu viwili vilivyofanya kazi pamoja hapo awali juu ya usajili wa alian Alvarez- unaipa timu ya Pep Guardiola mkono wa juu, kulingana na The Mirror.

Kifungu cha kuachiliwa kwa Echeverri ni pauni milioni 21.44, ingawa itaripotiwa kupanda hadi pauni milioni 25.73 ndani ya siku 10 za kufungwa kwa dirisha lolote la usajili.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 17 amefananishwa na Messi, lakini anasema: "Siku zote nilisema sanamu yangu ni Messi, lakini siko karibu na Messi!"

You Might Also Like

Get Newsletter

Advertisement