Septemba 19, 2022 ilikuwa ni siku nzuri kwa kiungo mshambuliaji, Issa Abushehe ‘Messi’ baada ya kupata dili la kujiunga na Al Mokawloon Al Arab inayoshiriki Ligi Kuu Misri akitokea Coastal Union ya Tanga.

Hata hivyo, baada ya dili kukamilika, huku wadau wa soka nchini wakimtabiria makubwa kutokana na uwezo alionao, ghafla msimu huu amerudi tena na kujiunga na Biashara United ya Mara iliyopo Ligi ya Championship.

SAFARI YA MISRI

Abushehe anasema baada ya kudumu kwa misimu minne Coastal ndipo ilikuja ofa ya kwenda Misri kwa ajili ya majaribio.

“Meneja wangu (Jamal Kajia) aliniambia Al Mokawloon inanihitaji na kama nitafanya vizuri katika majaribio basi watanisajili, nashukuru baada ya kufika kule nilifaulu na wakanisajili moja kwa moja, japo sikucheza,” anasema na kuongeza;

“Sikucheza kwa sababu wakati natoka Tanzania nilikuwa na jeraha la goti hivyo nilijitonesha na nilipofanyiwa vipimo nikatakiwa kufanyiwa upasuaji na nikatakiwa nikaa nje kwa miezi tisa na maisha yangu yakaanza kubadilika kuanzia hapo.”

You Might Also Like

Get Newsletter

Advertisement