Timu ya taifa ya marekani(USA) yaendelea kufanya vyema kwenye michezo yake yote ya kirafiki na kuonesha Dalili nzurii ya kuchukua ubingwa wa Olympic 

USA imecheza michezo mitatu ambayo ni Canada, Australia na Serbia lakini wameweza kushinda vizuri kabisa ambapo mwanzo waliaanza na Canada wakashinda mchezo wa pili na Australia akishinda mchezo wa 3 dhidi ya SERBIA ya Nikola Jokic wakafungwa 105-79 na ukwel timu hii ya USA inaonesha kutishia

Timu hii ya USA inafananishwa na ile ya mwaka 1992 wakati yupo Michael Jordan,Magic Johnson, Larry bird lakini ya mwaka 2008 wakati wa Kobe Bryant,Dawne Wade, Carmelo Anthony, Lebron James lakini timu ya MWAKA huu 2024 ikiongozwa na Lebron James, Curry, Durant, Davis,Adebayor, Edward,Booker,Tatum, White wanaonekana kuja kua tishiooo Sanaa 

Kumbuka miaka yote USA wakishiriki Olympic lazima atabeba Medal yoyote ile lakini pia USA ndio imechukua ubingwa mara nyingi Zaidi. 

Lakini kuelekea michuano hii ambayo inaenda kuanza juma lijalo siku ya ijumaa tarehe 26, taifa la USA limepata pigo la msiba la mchezaji wa zamani wa kikapu Mr JOE BRYANT baba mzazi wa Kobe Bryant akiwa na miaka 69. 

You Might Also Like

Get Newsletter

Advertisement