Mwanariadha nambari Tatu katika timu ya Olimpiki ya Wakimbizi Anjelina Nadai Lohalith amesimamishwa ili kusubiri kupimwa dawa za kusisimua misuli, huku tangazo hilo likija siku mbili kabla ya IOC kuthibitisha uteuzi wake wa wanariadha kwa ajili ya Michezo ya Olimpuki, Paris nchini Ufaransa.

Anjelina Lohalith alifahamishwa kuhusu madai yake ya matumizi ya dawa za moyo zilizopigwa marufuku, trimetazidine, na alisimamishwa kwa muda. 


Lohalith, ambaye alikimbia vita nchini Sudan Kusini akiwa mtoto na kukimbilia katika kambi ya wakimbizi nchini Kenya, alikuwa akifadhiliwa na Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki kujiandaa kwa Michezo yake ya tatu mfululizo ya Majira ya joto.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 31 alikimbia mbio za mita 1,500 kwa timu ya Wakimbizi katika Michezo miwili iliyopita ya Majira ya joto, akishindana kwa mara ya kwanza mwaka wa 2016 huko Rio de Janeiro na Olimpiki ya Tokyo 2021.

IOC na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi (UNHCR) wamepanga kukamilisha uteuzi wa timu ya wakimbizi kwa ajili ya Michezo ya Olimpiki ya Paris itakayofanyika kuanzia Julai 26 hadi Agosti 11.

Lohalith aliwakilisha Timu ya Wakimbizi katika Mashindano matatu ya Riadha ya Dunia na alikuwa mmoja wa wanachama 29 wa Timu ya Olimpiki ya Wakimbizi huko Tokyo.

UNHCR ilisema wanariadha 75 katika michezo 14 walipata ufadhili wa masomo kwenda Paris ambapo wanariadha hao wanatoka nchi 12 tofauti na sasa wanaishi katika nchi 24 zinazoandaa.


Mwanariadha wa ufadhili wa masomo kutoka Morocco ambaye pia ni mwanariadha wa mbio za mita 3,000 kuruka viunzi na maji Fouad Idbafdil, Mwezi Disemba alifungiwa kwa muda miaka mitatu baada ya kugundulika kuwa na virusi vya EPO.

Mnamo mwezi Machi mkimbiaji mwingine wa mita 1,500 kutoka Sudan Kusini, Dominic Lokolong Atiol, pia alisimamishwa kwa muda kwa kupimwa na kukutwa na trimetazidine.

Dawa hiyo inayojulikana kwa jina la TMZ, pia ilipatikana katika vipimo vya hali ya juu mwaka 2021 na mwanariadha (Gymnastics Girl ) kutoka nchini Urusi Kamila Valieva na waogeleaji 23 kutoka nchini China waliokuwa wakijiandaa kwa Michezo ya Olimpiki ya Tokyo.

Kesi ya Valieva ilikuja kujulikana wakati wa Michezo ya Majira ya baridi ya 2022 huko Beijing, ambapo aliwasaidia Warusi kushinda medali ya dhahabu ya timu.


Valieva baadaye alikataliwa, akasimamishwa kwa miaka minne, na Warusi walishushwa daraja hadi waogeleaji wa shaba, huku Merika ikipandishwa cheo na kuwa waogeleaji wa juu ambapo Kesi hiyo inaendelea na rufaa zaidi zinaendelea.

Swala la kuogelea la China lilielezewa kwa kina mnamo Aprili 20 katika ripoti za uchunguzi kutoka New York Times na shirika la utangazaji la Ujerumani ARD.

Waogeleaji hawakusimamishwa kazi, na watatu kati yao walijishindia medali za dhahabu mjini Tokyo, kwa sababu Shirika la Kupambana na Dawa za Kulevya Ulimwenguni lilikubali maelezo na ushahidi uliotolewa na mamlaka ya Uchina kwamba wanariadha hao walikuwa wameambukizwa na chembechembe za dawa hiyo kwenye jiko la hoteli.

You Might Also Like

Get Newsletter

Advertisement