Mwanamichezo wa Algeria Kaylia Nemour amefanikiwa kubeba Medali ya Dhahabu katika fainali ya mchezo wa Gymnactic (Kunyumbulika) kwa wanawake huko Paris 2024 na kuwa Mwafrika wa kwanza kabisa kushinda medali ya Olimpiki katika mazoezi ya viungo vya kisanaa.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 17 alikuwa ameongoza alama za kufuzu na kuboresha uchezaji huo kwa alama 15.700 kutoka kwa waamuzi kufuatia utaratibu wa haraka usio na dosari ambao ulikuwa na ujanja changamano wa kutolewa na kukamata.

"Nimeshtuka sana, ni ndoto ya maisha yangu yote. Siamini kuwa imetokea, sina la kusema," alisema.

Mafanikio ya Nemour pia yaliipatia Algeria dhahabu yake ya sita ya Olimpiki tangu iliposhiriki kwa mara ya kwanza Tokyo mnamo mwaka 1964.

Taifa la Afrika Kaskazini lilishika nafasi ya kwanza katika mashindano ya Olimpiki ya London 2012, wakati Taoufik Makhloufi aliposhinda mbio za mita 1500 kwa wanaume.

Mwaka jana Nemour, ambaye alizaliwa Saint-Benoit-la-Foret, Ufaransa, alikua Mwafrika wa kwanza kushinda medali ya ubingwa wa dunia katika mchezo wa gymnastics alipotwa Medali ya Fedha katika fainali ya uneven baa huko Antwerp.

Bingwa mtetezi wa Olimpiki, Nina Derwael wa Ubelgiji, alimaliza mashindano hayo katika nafasi ya nne.

Nemour alibadilika na kuiwakilisha Algeria, nchi alikozaliwa babake, mwaka jana baada ya mzozo na shirikisho la mazoezi ya viungo la Ufaransa kuhusu kurejea uwanjani kufuatia jeraha la goti.

You Might Also Like

Get Newsletter

Advertisement