Mabingwa watetezi Ivory Coast watakuwa na uhakika wa kufika fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika 2025 nchini Morocco lakini Nigeria wamewekwa katika kundi gumu katika droo ya kufuzu.

Droo iliyofanyika jijini Johannesburg iliwafanya Super Eagles kumenyana na Benin, Rwanda na Libya.

Benin, ambayo sasa inanolewa na kocha wa zamani wa Nigeria, Gernot Rohr, iliwashinda majirani zao 2-1 mwezi uliopita wakati timu hizo zilipokutana katika kufuzu kwa Kombe la Dunia la Fifa 2026.

Nigeria inatafuta meneja mpya baada ya Finidi George kujiuzulu kama kocha baada ya kushindwa na kujiunga na klabu ya Rivers United - ingawa shirikisho la soka nchini humo bado halijathibitisha rasmi kuondoka kwake.

Ivory Coast, ambayo ilishinda taji lao la tatu la bara mwezi Februari ilipoifunga Nigeria katika fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon) iliyocheleweshwa 2023, itamenyana na mabingwa wa 2012 Zambia, Sierra Leone na Chad.

Droo ya Afcon 2025

Kundi A:Tunisia, Madagascar, Comoros, The Gambia.

Kundi B:Morocco, Gabon, Central African Republic, Lesotho.

Kundi C:Egypt, Cape Verde, Mauritania, Botswana.

Kundi D:Nigeria, Benin, Libya, Rwanda.

Kundi E:Algeria, Equatorial Guinea, Togo, Liberia.

Kundi F:Ghana, Angola, Sudan, Niger.

Kundi G:Ivory Coast, Zambia, Sierra Leone, Chad.

Kundi H:DR Congo, Guinea, Tanzania, Ethiopia.

Kundi I:Mali, Mozambique, Guinea-Bissau, Eswatini.

Kundi J:Cameroon, Namibia, Kenya, Zimbabwe.

Kundi K:South Africa, Uganda, Congo, South Sudan.

Kundi L:Senegal, Burkina Faso, Malawi, Burundi.

You Might Also Like

Get Newsletter

Advertisement