Raundi ya 32 bora ya Kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) inaendelea leo kwa michezo minne kupigwa ambapo macho na masikio yatakuwa Uwanja wa Azam Complex itakapopigwa mechi kati ya Yanga na Polisi Tanzania kuanzia saa 12:00 jioni.

Kitakwimu na timu zinavyoonekana hii ni mechi ya mabao. Katika Championship, Polisi Tanzania imekuwa dhaifu kiulinzi kwani katika michezo 22 imeruhusu mabao 23 ikiwa ni wastani wa bao moja katika kila mechi tofauti na Yanga ambayo imefunga 39 na kuruhusu manane kwenye michezo 16.

Yanga ambao ndio mabingwa watetezi wanaingia wakiwa na kumbukumbu nzuri ya kushinda kwa mabao 3-0, mechi iliyopita na KMC huku kwa upande wa Polisi ikitoka kuchapwa 2-0 na Biashara United wiki iliyopita.

Mchezo huo huenda ukawa na mabadiliko kadhaa ya wachezaji kwa Yanga kutokana na mechi ijayo ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya CR Belouizdad kutoka Algeria itakayopigwa Jumamosi, Uwanja wa Mkapa.

You Might Also Like

Get Newsletter

Advertisement