Klabu ya Kaizer Chiefs imethibitisha kifo cha Nguli wa soka wa Afrika Kusini, Stanley ‘Screamer’ Tshabalala aliyefariki Dunia jana Julai 12, 2024 akiwa na umri wa miaka 75 kufuatia majeraha aliyopata baada ya kupigwa risasi alipovamiwa nyumbani mnamo Machi.


Tshabalala alikuwa gwiji ndani na nje ya uwanja huko Bondeni ambaye ni mwanachama na mwanzilishi wa Kaizer Chiefs. Alipewa jina la 'Screamer' kwa mtindo wake wa kuzungumza kwa sauti kubwa akiwa uwanjani enzi za uchezaji wake.

Baadaye, alifundisha klabu ya Mamelodi Sundowns, alijulikana kama 'Piano' na 'Shoe-shine' mtu, akiunda mtindo wa timu ya rhythm.

Ikithibitisha kifo hicho klabu ya Kaizer Chiefs imesema: “Familia ya Tshabalala na Orlando Pirates inatangaza kifo cha kusikitisha na kisichotarajiwa cha Stanley Tshabalala"

“Familia ya Tshabalala na Orlando Pirates itatoa maelezo kwa wakati ufaao. Umma unashauriwa kusubiri utoaji wa maelezo kwa ajili ya mipango inayoendelea,” imehitimisha taarifa hiyo.

You Might Also Like

Get Newsletter

Advertisement