KLABU ya Simba imelamba dili nono ya Sh 4 Bilioni baada ya kuingia mkataba mpya wa miaka miwili wa makubaliano ya kutengeneza na kusambaza jezi na Kampuni ya Sandaland Fashion Wear Limited.


Mkataba huo umesainiwa jana jijini Dar es Salaam baada ya klabu hiyo kumalizana na Kampuni ya Vunja Bei iliyoingia nao miaka miwili iliyopita ukiwa na thamani ya Sh 2 Bilioni.


Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano ya Simba, Ahmed Ally, aliliambia Mwanaspoti jana kuwa, wameamua kuingia mkataba na Sandaland baada ya kuvutiwa na ofa yao iliyokuwa mara mbili na ile iliyopita ya Vunja Bei.

You Might Also Like

Get Newsletter

Advertisement