Rais wa Kenya William Ruto, alituma wataalamu katika nyumba ya marehemu aliyeshikilia rekodi ya dunia ya kukimbia Kelvin Kiptum na kuwapa maagizo ya kumjengea nyumba ya vyumba vitatu mjane na watoto wake.

Ruto aliwaagiza wataalamu hao kujenga jumba hilo ndani ya siku saba kabla ya mazishi ya mwanariadha huyo kufanyika Februari 24.

Mkuu wa Nchi anatarajiwa kusimamia shughuli ya kukabidhi nyumba kwa mjane na watoto wa Kiptum kabla ya marehemu kuzikwa.

You Might Also Like

Get Newsletter

Advertisement