Pep Guardiola aliwaonya wakosoaji wa Erling Haaland "atawafunga mdomo" baada ya raia huyo wa Norway kuongeza matumaini ya Manchester City kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Uingereza.

Bao la ushindi la Haaland la dakika ya 71 dhidi ya Brentford lilisogeza City hadi nafasi ya pili kwenye jedwali - pointi moja tu nyuma ya viongozi Liverpool - huku akijibu kwa msisitizo kwa kukosa nafasi nyingi katika sare ya Jumamosi na Chelsea.

Pigo hilo la Chelsea lilikuja siku chache baada ya bibi yake Haaland kufariki, na meneja wa City Guardiola alichukua fursa hiyo baada ya mechi kutoa mawazo yake juu ya wakosoaji wa hivi majuzi - na waandishi wa habari.

“Ukiwa na wafungaji bora au washambuliaji wanaofunga mabao mengi, usilaumu kwa sababu atakufunga mdomo, hilo ni la uhakika,” alisema Guardiola. "Mapema au baadaye’’.

"Bila shaka, ikiwa nitachagua [mshambuliaji mwenye uwezo wa wa kukimbia kwenye goli], ninachagua huyu.

"Alikuwa nje na jeraha kwa miezi miwili na hayuko katika hali yake nzuri na alikuwa na wiki ngumu sana kwa sababu alimpoteza bibi yake. Hiyo si rahisi kwa binadamu."

Guardiola, ambaye alisema hataki kamwe kuwa mwandishi wa habari, aliulizwa ni nini kibaya kwa kuwa mmoja na majibu yake yalikuwa ya haraka.

"Mimi ni meneja," alisema. "Maisha yangu ni bora kuliko yako."

You Might Also Like

Get Newsletter

Advertisement