TIMU ya Ihefu imefuzu hatua ya nusu fainali ya michuano ya Kombe la Shirikisho (FA) baada ya kuifunga Mashujaa kwa mikwaju ya penalti 4-3, kufuatia miamba hiyo kutoka suluhu ndani ya dakika 90 kwenye Uwanja wa Liti, mjini Singida.

Nusu fainali itapigwa Mei 18 hadi 19 huku fainali ikipigwa Juni 2, mwaka huu kwenye Uwanja wa Tanzanite, uliopo Babati Manyara.

Mbali na Yanga ila timu nyingine iliyofika hatua hii na kuchukua ubingwa wa michuano hiyo ni Azam FC iliyofanya hivyo msimu wa 2018-2019 baada ya kuifunga Lipuli ya Iringa kwa bao 1-0, mechi iliyopigwa Uwanja wa Ilulu uliopo mjini Lindi.

Ihefu ilifika hatua hiyo kwa kuiondoa KMC katika hatua ya 16 bora kwa kuitandika mabao 3-0 huku Mashujaa ikiitoa Simba kwa penalti 6-5 kufuatia kufungana bao 1-1 ndani ya dakika 90 za mchezo huo uliopigwa Uwanja wa Lake Tanganyika, mjini Kigoma.





You Might Also Like

Get Newsletter

Advertisement