Mshambulizi wa zamani wa Brazil Romario ameacha kustaafu akiwa na umri wa miaka 58 na kusajiliwa kuchezea Klabu ya Soka ya Marekani pamoja na mwanawe.

Romario, ambaye alishinda Kombe la Dunia la 1994, ni rais wa timu yenye maskani yake Rio de Janeiro, ambayo inacheza katika daraja la pili la mashindano ya kanda ya Rio.

Romario alisema hatacheza ligi, lakini alitaka kushiriki katika baadhi ya michezo pamoja na mwanawe Romarinho.


Romario alicheza mchezo wake wa mwisho mnamo Novemba 2009.

Uchezaji wake ulianza mwaka 1985 akiwa na Vasco de Gama kabla ya kucheza vyema Uholanzi akiwa na PSV na Barcelona ya Uhispania.

Alistaafu mnamo 2009, akicheza mchezo wake wa mwisho katika klabu ya Amerika FC, ambapo baba yake Edevair alicheza, kabla ya kuchaguliwa kuwa seneta wa Rio de Janeiro mnamo 2014.


Alifunga mabao 55 katika mechi 70 alizoichezea Brazil, na alichaguliwa kuwa mchezaji bora wa mwaka wa Fifa mwaka wa 1994 baada ya kufunga mabao matano katika kampeni yao ya kushinda Kombe la Dunia.

You Might Also Like

Get Newsletter

Advertisement