Mohamed Salah "alikosea" kwa kuzozana na meneja wa Liverpool Jurgen Klopp kwenye mstari wa kutoka nje ya uwanja wakati wa sare ya 2-2 Jumamosi dhidi ya West Ham United,

amesema mshambuliaji wa zamani wa Ligi ya Premia Chris Sutton.

Salah alikuwa amekalia benchi katika mchezo huo na akagombana na Klopp huku akijiandaa kuingia kama mchezaji wa akiba katika dakika ya 79.

Sare hiyo inawaacha Liverpool, ambao wako nje ya Ligi ya Europa, pointi tano nyuma ya vinara wa Ligi Kuu, Arsenal.

Sutton anasema tukio hilo halikumuonyesha vyema mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 31, ambaye ni mfungaji bora wa Reds msimu huu akiwa na mabao 24 lakini hajakuwa katika kiwango bora katika michezo ya hivi majuzi.

"Sikupenda lakini nadhani Mo Salah ndiye aliyekosea" Sutton alisema kwenye kipindi cha Jumatatu Usiku cha BBC Radio 5 Live.


"Hana tofauti na wachezaji wenzake wa Liverpool na ukweli ni kwamba kiwango chake hakijakuwa kizuri tangu aliporejea kutoka kwenye jeraha.

"Sina ubaya dhidi ya Salah na mchezaji mahiri ambaye amekuwa Liverpool. Amekuwa wa ajabu lakini nadhani kuna mstari na kwa bahati mbaya aliuvuka."

Klopp, ambaye anaondoka Liverpool mwishoni mwa msimu, alimleta Salah Anfield mnamo Juni 2017 na amekuwa mmoja wa wachezaji wake wenye ushawishi mkubwa.

Lakini Sutton anaamini kuwa Klopp alikuwa na kuchagua kikosi chake cha wachezaji XI wa kwanza aliohisi kuwa waliipa Liverpool nafasi nzuri zaidi ya kupata ushindi.

You Might Also Like

Get Newsletter

Advertisement