LIGI kuu ya NBC Tanzania bara inaendelea tena leo Aprili 23 kwa mechi moja ambapo Wananchi Young Africans Sc watakuwa kibaruani katika jitihada za kuendelea kuusogelea ubingwa wa Ligi 2023/24.

JKT Tanzania ambapo wapo nafasi moja kutoka mkiani wakiwa na alama 22 baada ya mechi 22 wanatafutu ushindi wa kwanza ndani ya mwaka 2024 wakishindwa kupata ushindi kwenye mechi 14 za michuano yote.

Wananchi wanahitaji ushindi kwa ajili ya kuendelea kujichimbia zaidi kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ambapo kwa sasa wapo kileleni alama 58 baada ya mechi 22.

You Might Also Like

Get Newsletter

Advertisement