Kocha wa Barcelona Xavi atasalia katika klabu hiyo hadi mwisho wa mkataba wake mnamo Juni 2025 baada ya kubadilisha mawazo kwamba huu ungekuwa msimu wake wa mwisho.

Kocha huyo mwenye umri wa miaka 44 alitangaza Januari kwamba atajiuzulu kama bosi msimu huu wa joto.

Lakini, huku rais Joan Laporta akitamani abaki, kiungo huyo wa zamani wa Barcelona na Uhispania amebatilisha uamuzi wake.

Xavi alichukua nafasi hiyo Novemba 2021 baada ya kuachana na klabu ya Al Sadd ya Qatar na kuiongoza Barca kutwaa ubingwa wa Uhispania katika msimu wake wa kwanza kamili wa kuinoa klabu mnamo 2022-23.

Hata hivyo, wako pointi 11 nyuma ya vinara wa La Liga Real Madrid zikiwa zimesalia mechi sita kuchezwa katika msimu unaoendelea.

Barcelona iliondoka kwenye Ligi ya Mabingwa wiki iliyopita kufuatia kushindwa katika robo fainali na Paris St-Germain.

Xavi, ambaye alishinda tuzo 25 wakati wa uchezaji bora katika klabu ya Barcelona, ​​alisema anahisi "amefunguliwa" kufuatia tangazo kwamba atajiuzulu nafasi hiyo mwishoni mwa msimu.

Alipotangaza kuwa anaondoka baada ya kushindwa na Villarreal, alihisi kwamba halindwi na klabu hiyo na hakukuwa na mwelekeo wazi.

Lakini tangu wakati huo, Xavi alipohisi anaweza kuchukua mbinu ya utulivu zaidi, matokeo ya timu yaliboreka.

Barcelona walicheza mechi 10 bila kufungwa kwenye ligi kabla ya kufungwa 3-2 na Real Madrid Jumapili.

You Might Also Like

Get Newsletter

Advertisement