KOCHA NABI RASMI NI KOCHA MKUU WA KIKOSI CHA KAIZER CHIEFS (AMAKHOSI) KWA MSIMU UJAO
TIMU ya Kaizer Chief ya pale South Africa imefanikiwa kunasa Saini ya Kocha wa As Far RABAT ya pale Morocco hivyo atakua katika benchi la ufundi la Kaizer Chief
Sasa mbali na Kocha NABI timu hiyo ya Kaizer Chief imeweza kumsajili pia kocha FERNANDO DA CRUZ raia wa Ufaransa kwenda kushirikiana na Kocha NABI
SASA Kocha NABI na Fernando da Cruz wote itakua pair ambayo itaungana kujenga Kaizer Chief MPYA yenye ubora mkubwaa watu wanasubiri hii pair ya Tunisia na Ufaransa je itafanikiwa
Kumbuka makocha hawa wote wataondoka As Far RABAT kutoka pale Morocco mara baada ya kutamatika kwa michuano ya Throne cup basi wataenda kujiunga na Kaizer Chief, Mafanikio makubwa pale ni kumaliza nafasi ya pili na kwenda klabu bingwa Africa
Ujio wa Kocha NABI na Fernando da Cruz nidhahiri ule uvumi wa kocha PITSO JOHN HAMILTON MOSEMANE umekufa kwani Kocha PITSO alikua ndo anapewa kipaumbele kwel kwel lakini NABI ndio amekua chaguo la kwanza