Idadi hiyo inawakilisha ongezeko la 43% kwenye dola $623m (£493m) iliyotumiwa mwaka wa 2022 na kupita rekodi ya awali ya dola $655m (£518m) kutoka 2019.

Vilabu vya Uingereza ndivyo vilivyotumia pesa nyingi zaidi mwaka huu na dola $280m (£221m).

Zaidi ya dola $1m (£790,000) zilitumika kulipa ada za mawakala katika soka ya wanawake kwa mara ya kwanza.

Ripoti ya Mawakala wa Soka katika Uhamisho wa Kimataifa inasema kulikuwa na rekodi ya mikataba ya kimataifa 3,353 mwaka huu.

Haijumuishi uhamisho wa ndani kama vile uhamisho wa Declan Rice wa euro £100m kutoka West Ham kwenda Arsenal na Moises Caicedo kuondoka Brighton kwenda Chelsea kwa euro £100m.

Harry Kane aliondoka Tottenham na kwenda Bayern Munich kwa euro £86m na Jude Bellingham akajiunga na Real Madrid kutoka Borussia Dortmund kwa euro £89m.

Ripoti hiyo inaonyesha vilabu barani Ulaya vilichangia 87% ya matumizi ya mawakala mnamo 2023.

Vilabu vya Saudi Pro League vilitumia dola $86m (£68m), huku Karim Benzema, Sadio Mane na Riyad Mahrez wakiwa miongoni mwa wachezaji waliohama.

Korea Kusini ilikuwa na sehemu kubwa zaidi ya uhamisho unaoondoka, huku mawakala wanaohusika na uuzaji wa vilabu katika Ligi wakiwa 32% ya jumla iliyotumika.

Vilabu vya wanawake vilitumia karibu dola $1.4m (£1.1m) kwa mawakala katika rekodi ya uhamisho 125.

You Might Also Like

Get Newsletter

Advertisement