Klabu ya Nottingham Forest inayoshiriki Ligi kuu nchini Uingereza imekatwa Pointi nne kwa kukiuka kanuni za Faida na uendelevu za Ligi kuu nchini humo (PSR).

Klabu hiyo ilishitakuwa mwezi Januari mwaka huu

Kwa kupunguzwa Pointi nne kunaiweka Klabu hiyo chini ya Luton Town wenye Pointi 22 na kuwa kwenye hatari ya kushuka daraja ambapo wanakuwa na Pointi 21.

Forest walipangwa kupunguzwa kwa pointi sita - pointi tatu kwa uvunjaji wa awali na tatu zaidi kwa ukubwa wa uvunjaji - lakini "maombi yao ya mapema" na "ushirikiano" ulipungua hadi pointi nne.

Forest ni timu ya pili ya ligi kuu kuadhibiwa kwa ukiukaji wa PSR baada ya Everton kupoteza pointi 10 mwezi Novemba, ambazo zilipunguzwa hadi sita baada ya kukata rufaa

You Might Also Like

Get Newsletter

Advertisement