Nyota wa soka wa Afrika Kusini Luke Fleurs ameuwawa katika tukio la uporaji gari, klabu yake ya Kaizer Chiefs imesema.

Mlinzi huyo mwenye miaka 24, alipigwa risasi na watu wanaodhaniwa kuwa ni waporaji wa magari, katika tukio lililotokea katika kituo cha mafuta eneo la Honeydew, mjini Johannesburg nchini Afrika Kusini.

"Luke Fleurs amefariki dunia katika tukio la uporaji mjini Johannesburg. Tunaungana na familia yake katika kipindi hiki kigumu," ilisema klabu ya Kaizer Chiefs kupitia taarifa yake.

Kwa mujibu wa msemaji wa Jeshi la Polisi la nchi hiyo Mavela Masondo, wauaji hao walitokomea na gari la Fleurs, mara baada ya kutekeleza mauaji hayo.

"Fleurs alikuwa anasubiri kuwekewa mafuta kabla ya kuvamiwa na watuhumiwa hao ambao walimpiga risasi kifuani huku mmoja akifanikiwa kukimbia na gari la mchezaji huyo," alisema Masondo.

Hakuna mtu aliyekamatwa kuhusiana na tukio hilo hadi sasa, limesema jeshi hilo.

Jitihada za kumuwahisha hospitali hazikuzaa matunda kwani alipoteza uhai wake mara tu baada kufikishwa hospitali.







You Might Also Like

Get Newsletter

Advertisement