Atletico Madrid Wameifunga Borussia Dortmund 2-1 na kuwa na faida ndogo baada ya mkondo wa kwanza wa robo fainali ya Ligi ya Mabingwa.

Kikosi cha Diego Simeone kilianza vyema uwanjani Estadio Metropolitano naye Rodrigo de Paul akawaweka mbele dakika ya nne baada ya kutumia vyema pasi ya Ian Maatsen.


Wageni walionekana kuwa na wasiwasi sana mapema na ilipoonekana wametulia kwenye mchezo, mchanganyiko mwingine katika safu ya ulinzi ulimruhusu beki wa pembeni Samuel Lino kuipata pasi ya Antoine Griezmann na kuifungia Atletico bao la pili kwa utulivu.



You Might Also Like

Get Newsletter

Advertisement