WAKATI ambao mashabiki wa Bayer Leverkusen wameusubiri kutoka kizazi kimoja kwen-da kingine.

Kutoka kutaniwa 'Neverkusen' hadi kubeba ubingwa wa Ligi Kuu Ujerumani maarufu kama Bundesliga 'what a moment'.

Hii ni sawa na mtumwa kutawazwa kuwa mfalme.

Imewezekanaje? Mbele ya Bayern Munich ambao wanaonekana kulitawala soka la Ujerumani kutokana na nguvu kubwa waliyonayo kiuchumi na Borussia Dortmund, huku Leverkusen ambayo msimu uliopita ilikuwa katika hatari ya kushuka daraja hadi kuwa timu tishio.



"Mzee wa mipango, mbunifu". Hayo ni machache kati ya maneno ambayo mashabiki wa Bayer Leverkusen walitumia kumuelezea Xabi Alonso, siku chache kabla ya mechi ya leo.

Chini ya usimamizi wake, klabu hiyo imeweka rekodi nyingi za kibabe ambazo ni kama utukufu kwenye taji la kifalme ambalo wamevalishwa leo, Jumapili baada ya kuwachapa mabingwa wa zamani wa ligi hiyo, SV Werder Bremen.

Kwanini waliitwa Neverkusen? Hilo lilikuwa jina la utani baada ya kukosa taji hilo katika mtindo wa kushangaza mwishoni mwa msimu wa 1999-2000 na 2001-2022, huku kikosi kikiwa na mastaa Michael Ballack, Jose Roberto da Silva Junio 'Ze Roberto', Paulo Roberto Rink na Adam Matysek.

Alonso ndiye kidume ambaye amebadili upepo wa mambo huko Ujerumani kwa Leverkusen ambayo wakati akipewa kibarua cha kuinoa timu hiyo Oktoba 5, 2022, kumrithi Gerardo Seoane hakuna ambaye alikuwa akidhani kuwa pengine msimu unaofuata Mhispania huyo angeweza kufanya balaa hili.



Aliikuta Leverkusen ikiwa nafasi ya pili kutoka mkiani baada ya michezo minane ya Bundesliga, ikiwa na mwanzo mbaya zaidi wa msimu tangu 1979.

Alikuwa na muda mfupi wa kuiandaa timu na mchezo wake wa kwanza ambao ulichezwa siku tatu baada ya kutambulishwa kwake, lakini kwa bahati nzuri Leverkusen iliibuka na ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Schalke 04.








You Might Also Like

Get Newsletter

Advertisement