Shirikisho la Soka la Kimataifa FIFA na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limeifungia klabu ya Yanga kusajili wachezaji wa kimataifa na wa ndani.

Mashirikisho hayo yamefikia uamuzi huo baada ya aliyekuwa mchezaji wa timu hiyo Lazarus Kambole kushinda kesi ya madai dhidi ya klabu hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa umma na TFF imesema Kambole aliishitaki Yanga kwa madai ya malimbikizo ya mshahara na fidia ya kuvunjiwa mkataba, ambapo timu hiyo ilipewa siku 45 kulipa pesa hizo na ilishindwa.


Taarifa hiyo imeeleza kuwa kushindwa kutekeleza hukumu ndani ya muda husika ndio sababu ya timu hiyo kufungiwa kusajili usajili wa ndani na wa nje.

Yanga ilimtambulisha Kambole raia wa Zambia Juni 16, 2022 akitokea Kaizer Chiefs ambapo Septemba,2022 iliachana na mchezaji huyo na kumpeleka kwa mkopo kwenye timu ya Wakiso Giant ya Uganda.

You Might Also Like

Get Newsletter

Advertisement