Kwa mujibu wa serikali ya Ivory Coast dola bilioni 1 zimetumika kuandaa mashindano hayo, ambayo yataanza Jumamosi, baada ya kujenga viwanja vinne vipya na kukarabati vingine viwili.

Aidha, viwanja vya ndege, barabara, hospitali na hoteli zimejengwa au kuboreshwa katika miji mitano itakayoandaa mechi; Abidjan, Bouake, Korhogo, San Pedro na Yamoussoukro.

Ni ujenzi mkubwa wa maendeleo katika taifa hilo la Afrika Magharibi tangu vita vya wenyewe kwa wenyewe 2002-2007 na 2010-11. Baadhi ya fedha za ujenzi zimetokana na mkopo wa dola za kimarekani bilioni 3.5 kutoka Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) Aprili mwaka jana.

Huku Ivory Coast ikiorodheshwa kama taifa la 138 kati ya 190 na IMF kwa ukubwa wa uchumi. Uchumi wake umekuwa kwa wastani wa 8% kwa mwaka tangu Rais Alassane Ouattara, mfanyakazi wa zamani wa IMF achukue madaraka 2010.

"Ivory Coast ni nchi maskini," Prao Yao Seraphin, profesa wa uchumi wa Ivory Coast, aliiambia BBC Sport Africa.

"Kutokana na hali hiyo, Rais Ouattara amelazimika kuchukua mikopo kufadhili mradi huu, hivyo tunapaswa kuhakikisha mikopo hiyo inanufaisha Ivory Coast. Nchi italazimika kutunza miundombinu."

Ivory Coast, ambayo wakati mmoja ilikuwa nyumbani kwa mojawapo ya idadi kubwa zaidi ya tembo barani Afrika – itakuwa mwenyeji wa kombe la Afrika mwaka huu.

You Might Also Like

Get Newsletter

Advertisement