Harry Kane anaonekana kuwa sawa kukabiliana na Arsenal katika Ligi ya Mabingwa mwezi ujao baada ya kurejea kwenye mazoezi mepesi na Bayern Munich.

 Kane alijiondoa kwenye kikosi cha Uingereza wiki iliyopita kwa sababu ya jeraha la kifundo cha mguu.

 Mshambuliji huyo wa zamani wa Tottenham alikosa kipigo cha Jumamosi cha 1-0 kutoka kwa Brazil na akarejea Ujerumani mwishoni mwa juma kuendelea na ahueni.   

Lakini Kane anatumai kurejea kwa wakati ili kuongoza nguvu kwa washambuliaji kwa Bayern watakapo safiri kwenda uwanja wa Emirates kwa mkondo wa kwanza wa robo-fainali ya Ligi ya Mabingwa mnamo Aprili 9.

Bayern ilithibitisha Jumatatu kwamba Kane amerejea kwenye mazoezi ya binafsi na wababe hao wa Bundesliga wanatumai atakuwepo kwenye mchezo wa Borussia Dortmund siku ya Jumamosi hii. 

 Arsenal itamenyana na Bayern wakati Kane atarejea kucheza kaskazini mwa London kwa mara ya kwanza tangu aondoke Tottenham majira ya joto yaliyopita.

You Might Also Like

Get Newsletter

Advertisement