Droo ya hatua ya 16 bora ya Ligi ya Mabingwa itafanyika Jumatatu, Disemba 18, huku klabu mbili za Uingereza zikisubiri kujua hatima yao.

Mabingwa Manchester City, na Arsenal, walishinda makundi yao na kutinga hatua ya mtoano, huku Newcastle, Manchester United na mabingwa wa Uskoti Celtic wakijipata nje.

Waliowekwa kwenye makundi: Arsenal, Atletico Madrid, Barcelona, Bayern Munich, Borussia Dortmund, Manchester City, Real Madrid, Real Sociedad.

Ambao hawajawekwa: Copenhagen, Inter Milan, Lazio, RB Leipzig, Napoli, Paris St-Germain, Porto, PSV Eindhoven.

Droo ya hatua ya 16 bora ya Ligi ya Mabingwa itafanyika Jumatatu, Disemba 18 saa 11:00 GMT katika ukumbi wa House of European Football huko Nyon, Uswizi.

Kila mshindi wa kundi atatolewa na kupangwa dhidi ya timu iliyoshika nafasi ya pili katika kundi jingine, ambao wote hawajapatikana. Timu haziwezi kuwekwa dhidi ya klabu zinazotoka nchi moja, au timu zilizokuwa kundi moja nazo.

Mechi za mkondo wa kwanza wa hatua ya 16 bora zitachezwa kwa wiki mbili, 13-14 na 20-21 Februari 2024, na marudiano 5-6 na 12-13 Machi.

Droo za robo fainali na nusu fainali zitafanyika kwa pamoja Ijumaa, Machi 15.

Manchester United walimaliza wa mwisho katika Kundi A baada ya vipigo vinne kutoka kwa mechi sita za kundi hilo.

Ilikuwa ni mara ya sita kwa Mashetani Wekundu kushindwa kutinga hatua ya mtoano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya na mara ya kwanza kumaliza mkiani mwa kundi lao tangu 2005-06.

Bayern Munich walitinga hatua ya 16 bora wakiwa washindi wa kundi wakiwa na mechi mbili zilizosalia, huku Copenhagen ikisonga mbele kwa awamu ya muondoano kwa mara ya kwanza tangu 2010-11.

Galatasaray ilitolewa katika raundi ya muondoano ya Ligi ya Europa

Arsenal walishinda kundi lao wakiwa na mchezo mmoja wa ziada na PSV Eindhoven pia wakimaliza katika nafasi ya pili baada ya mechi tano.

Lens iliepuka kushindwa na Sevilla katika mechi yao ya mwisho ili kujihakikishia nafasi ya kucheza Ligi ya Europa.

You Might Also Like

Get Newsletter

Advertisement