AL ITTIHAD ya Saudi Arabia imepanga kuongeza ofa ili kufikia Pauni 30 milioni kuhalikisha inaipata saini ya kipa wa Manchester City, Ederson Santana de Moraes maarufu kama Ederson katika dirisha lijalo la majira ya kiangazi.

Staa huyo wa kimataifa wa Brazil ameanza kuhusishwa na timu hiyo katika siku za karibuni kwa kile kinachoelezwa kwamba alipishana kauli na kocha Pep Guardiola ambaye ametoa ruhusa kama akipata timu aende.

Pia Ederson anataka kupata changamoto mpya na pesa nyingi zaidi ambazo Uarabuni amewekewa mezani.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka vyanzo mbalimbali Al Ittihad ambayo inamtaka na Mohamed Salah inataka kumpa Ederson mshahara unaofikia mara tatu zaidi ya ule anaoupata kwa sasa wa Pauni 180,000 kwa wiki.

Kipa huyo namba moja na tegemeo Man City mkataba wake unatarajiwa kumalizika 2026. Tangu kuanza kwa msimu huu amecheza mechi 43 za michuano yote, huku 26 akimaliza bila kufungwa.

You Might Also Like

Get Newsletter

Advertisement